Akiwasilisha takwimu za Ukatili na Udhalilishaji wa Kijinsia kwa wanawake na Watoto Mtakwimu Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali katika Kitengo cha Makosa ya Jinai,Madai na Jinsia Ramla Hassan Pandu wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko katika ukumbi wa Mtakwimu Mkuu wa Serikali uliopo Mazizini.
Amesema Mlinganisho wa idadi ya matukio kwa Mwezi imepungua kwa asilimia 11.1 kutoka matukio 108 kwa mwezi wa Julai,2021 hadi 96 mwezi wa Agosti 2021.
Aidha amesema Wilaya ya Magharibi “A” imeripotiwa kuwa na matukio mengi ukilinganisha na Wilaya nyengine ambapo matukio 25 ikifuatiwa na Wilaya ya Magharibi “B” Matukio 20 ambapo Wilaya ya Kaskazini “A” Micheweni na Mkoani zimeripotiwa kuwa na idadi ndogo zaidi ya matukio kuliko wilaya zote matukio mawili 2 kwa kila wilaya.
Muwasilishaji huyo amesema matukio 90 yapo chini ya upelelezi wa Polisi na matukio 6 yapo katika hatua nyengine ambapo matukio 4 manne yapo Mahakamani na matukio mawili 2 yapo Ofisi ya Mashitaka.
Kwa upande wake Mrakibu Msaidizi wa Polisi Mkuu wa Kitengo cha Takwimu Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Ramadhani Himidi amesema Jeshi la Polisi linatoa wito kwa jamii kuendelea kushirikiana katika kutokomeza vitendo vya udhalilishaji ili viweze kumalizika.
Nae Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii Wanawake na Watoto kutoka Kitengo cha Watoto Mohamed Jabir amesema ili tatizo hilo lisiendelee taaluma itolewe kwa wazazi wawe karibu na watoto na kuwaelimisha ili waweze kujinusuru pale watapofikwa na kadhia hiyo waweze kuepukana nayo.