SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar inalaani vikali tukio
la kupigwa kwa mwanasiasa mkongwe Bwana Baraka Mohamed Shamte lililotokea hapo jana.
Katika tukio
hilo inasemekana kwamba mwanasiasa huyo amejeruhiwa katika baadhi ya sehemu
zake za mwili tukio ambalo lilipelekea kupata maaumivu makali na hatimae
kukimbizwa hospitali.
Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar inatoa pole kwa mwanasiasa huyo mkongwe na kuahidi kwamba
inalichunguza tukio hilo na kuhakikisha kupitia vyombo vyake vya ulinzi na
usalama vinawatia mbaroni wahusika.
Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar inapinga vitendo vya watu kujichukulia sheria mikoni na
kuwataka watu kuwa watulivu wakati vyombo husika vinalifanyia kazi suala hilo.